Tuesday, April 20, 2010

wakazi wa mpitimbi

Wakazi wa kijiji hiki wengi wao ni Wangoni lakini wapo pia, ingawa wachache, Wanyasa, Wamatengo, Wabena, Wapangwa kwa kuyataja machache. Majina ya ukoo ya kina Mbawala, Komba, Nyoni, Haule, Mbena, Matembo, Mbeyu, Ngaponda, Ndauka, Kapinga, Chale, Ngonyani, Mapunda, chipeta, Kihwili, Mkinga, Mbawa, Mgomela, Nyirenda, Miti, Soko ni ya kawaida kabisa.

Wakazi hawa wanajishughulisha zaidi na kilimo. Miongoni mwa mazao wanayolima ni pamoja na mahindi, tumbaku, soya, ulezi, alizeti, nk.

Vyakula vya pekee vinavyopatikana Mpitimbi, ambavyo wanampitimbi waliopo Diaspora wanavimisi ni kikande, mawungu, mapotopoto a.k.a masuku, mapondo, mabuni, vipwete, madonga, ngumbi a.k.a mbulika, mangatungu, mafiwi nk.

1 comment: